Ubelgiji Yatinga Robo Fainali Kombe La Dunia..... Ilipigwa 2-0 na Japan, Ikaamka Na Kushinda 3-2
Ulihitajika
moyo wa chuma kuamini Ubelgiji wangetoboa. Ilikuwa ni zaidi ya mechi ya
hatua ya 16. Ilikuwa ni kufa na kupona. Ulikuwa ni ubabe. Baada ya
kushuhudia wakipigwa 2-0 ndani ya dakika nne, ubelgiji waliishangaza
dunia.
Katika
mchezo mkali pengine kuliko yote yaliyoshuhudiwa kwenye fainali za
mwaka huu, Ubelgiji walijikuta wakipigwa bao la kwanza katika dakika ya
48 Genki Haguchi kupiga shuti kali lililomzidi ujanja kipa wa Ubelgiji,
Thibaut Coutouis kabla Takashi Inui hajaiweka Japan mguu mmoja ndani ya
robo fainali, katika dakika ya 52.
Japan
wakiamini wamemaliza biashara iliyowapeleka katika uwanja wa Rostov
Don, Kocha wa Ubelgiji, Roberto Martinez alifanya maamuzi ya kijasiri
ambayo mwisho wa siku yaliiokoa Ubelgiji. Mhispania huyo baada ya kuona
kikosi chake kimezidiwa, aliamua kuwatoa Ferreira Carrasco na Dries
Martens kwa mpigo.
Akawaingiza Nacer Chadli na Maroune Fellaini. Wote hawa ni warefu.
Kuanzia hapo Ubelgiji ni kama walizaliwa upya kabisa. Wakapiga mpira mwingi na kuwapoteza Samurai Blue kabisa. Katika dakika ya 69, Jan Vertonghen alipiga krosi iliyotinga nyavuni moja kwa moja.
Kuanzia hapo Ubelgiji ni kama walizaliwa upya kabisa. Wakapiga mpira mwingi na kuwapoteza Samurai Blue kabisa. Katika dakika ya 69, Jan Vertonghen alipiga krosi iliyotinga nyavuni moja kwa moja.
Dakika
tano baadaye, Fellaini akasawazisha kwa kichwa safi akiunganisha krosi
ya Eden Hazard, huku la tatu na ushindi likiwekwa kambani na Nacer
Chadli, kufuatia shambulizi la kushtukiza, kunako dakika ya 90. Mwisho
wa siku ndio kama mlivyosikia, Ubelgiji wakashinda 3-2.
Licha
ya kuwapa tiketi ya kuwafuata Brazil kibabe, Ubelgiji waliweka rekodi
ya kuwa timu ya kwanza kufufuka na kushinda mechi ndani ya dakika 90,
baada ya kutanguliwa kwa mabao mawili au zaidi, tangu Ureno wafanye
hivyo miaka 52 iliyopita. Mwaka 1966, Ureno walitoka nyuma na kuinyuka
DPR Korea 5-3, baada ya Korea kutangulia kupata mabao matatu ya haraka.
Aidha
ushindi huo, unamaanisha kuwa, Ubelgiji wamefuzu hatua ya robo fainali
ya Kombe la Dunia mara mbili mfululizo kwa mara ya kwanza. Hata hivyo,
mabao mawili waliyofungwa na Japan yalimaanisha kuwa, Ubelgiji
hawajawahi kumaliza mechi bila kufungwa katika mechi 12 za Kombe la
Dunia, walizocheza kwenye hatua ya mtoano.
No comments: